Habari Kutoka Ubalozi
Wachangiaji Damu: Mashujaa Wanaookoa Maisha
June 13, 2013
Kila mmoja wetu, katika wakati mmoja au mwingine wa maisha yake anaweza kukabiliana na janga lisilotarajiwa. Ajali za barabarani, upungufu wa damu utokanao na malaria au matatizo ya uzazi yanaweza kutokea wakati wowote na kuhitaji jitihada za haraka za kuokoa maisha. Jitihada hizi zinaweza kuwa ni zile zinazotegemea tu upatikanaji wa kundi sahihi la damu kutoka katika benki ya damu. Kwa bahati mbaya sana, mara nyingi ukosefu wa damu husababisha vifo ambavyo vingeweza kabisa kuepukika. Kutokana na hali hiyo, mara nyingi kitendo cha mgonjwa kuwekewa damu ni jambo linalotofautisha uzima na kifo... (Habari Zaidi)
-
Tamko la Msemaji wa Ikulu ya Marekani kuhusu Ziara ya Rais Barani Afrika
Kuanzia tarehe 26 Juni hadi 3 Julai, Rais Obama na Mkewe wanatarajia kutembelea nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania. Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi... Habari Zaidi »
-
Kulinda uhuru wa vyombo vya habari huimarisha demokrasia
Mojawapo kati ya vielelezo muhimu vya jamii ya kidemokrasia ni kuwepo kwa vyombo vya habari vilivyo imara na huru. Katika nchi ya kidemokrasia ni lazima raia wawe na uwezo wa kujadili masuala mbalimbali kwa uwazi, kwa amani na bila hofu yoyote... Habari Zaidi »
-
Wajasiriamali Wanawake Waanzisha Tawi hapa nchini
Wajasiriamali wanawake wa Kitanzania waliowahi kushiriki katika Programu ya Wajasiriamali Wanawake wa Kiafrika inayoendeshwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani wameanzisha tawi la Tanzania la Chama cha Wajasiriamali Wanawake wa Afrika (AWEP). Tawi hilo limezinduliwa leo katika hoteli ya Doubletree, Hilton jijini Dar es Salaam... Habari Zaidi »
-
Balozi Lenhardt atoa tuzo kwa wanawake Jasiri wa Kitanzania
Hapo tarehe 4 Aprili, Balozi wa Marekani nchini Alfonso E. Lenhardt alitunuku tuzo ya Wanawake Jasiri wa Kitanzania kwa Mwaka 2013 kwa Mheshimiwa Fatma Abdulhabib Fereji, Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Muungano wa Kitaifa ya Zanzibar na Bi. Ndinini Kimesera Sikar, Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Wanawake wa Kimaasai (MWEDO) katika hafla iliyofanyika katika Ubalozi wa Marekani.... Habari Zaidi »
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Marekani azindua Kituo cha Wageni katika Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Burunge
Jumanne, Februari 5, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Marekani David J. Hayes alikabidhi usimamizi wa kituo cha wageni katika hifadhi ya wanyamapori inayosimamiwa na jamii (Wildlife Management Area- WMA) ya Burunge, wilayani Babati, mkoani Manyara kwa Waziri wa Maliasili na Utalii.... Habari Zaidi »
Ripoti
-
Ripoti za Nchi Kuhusu Mwenendo wa Haki za Binadamu (2012)
(Adobe Acrobat - 273kb)
Imetolewa na Ofisi ya Demokrasia, Haki za Binadamu na Kazi ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani
May 2013