Siku ya Jumatano Januari 10 mwaka huu, Balozi wa Marekani nchini Michael L. Retzer aliungana na Mbunge wa Marekani Steven Weickert kutoka Appleton, Wisconsin, pamoja na Wamarekani wengine 14 wa kutoka jimbo la Wisconsin, ambao hivi sasa wanatembelea Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga kusaidia kujenga nyumba kwa watu wanaohitaji makazi. Mradi huu ni sehemu ya mpango wa taasisi ya Habitat for Humanity Tanzania unaolenga kujenga nyumba nzuri zenye gharama nafuu kwa wananchi wa Korogwe, ambao hawana nafasi ya kupata makazi ya kuridhisha.
|