Skip Navigation
Skip Left Section Navigation

Matukio Katika Picha

Mzee Kawawa atunukiwa tuzo ya kumuenzi Dk. Martin Luther King Jr.

 

Jumanne Januari 23, 2007 mwanasiasa mkongwe Mzee Rashid Mfaume
Kawawa, alitunukiwa tuzo ya kumuenzi Dk. Martin Luther King inayojulikana
kama Martin Luther King Jr. Drum Major for Justice Award, kwa
mchango wake mkubwa kwa taifa la Tanzania, kabla na baada ya uhuru wa
nchi hii. Mzee Kawawa alitunukiwa tuzo hiyo na Balozi wa Marekani nchini
Michael L. Retzer.
Tuzo ya Drum Major for Justice Award ilianzishwa ili kumuenzi Dk.
Martin Luther King, Jr. Dk. King alikuwa mtu mashuhuri katika nyakati za
historia ya hivi karibuni. Hotuba na mihadhara yake ilichochea dhamira ya
kizazi kizima. Harakati na maandamano aliyoyaongoza yalileta mabadiliko
muhimu katika mfumo wa maisha nchini Marekani, kupitia ujasiri na
msimamo wake thabiti wa kujitoa. Msimamo huu ndio uliongoza harakati za
kupigania haki za raia kwa miaka kumi na mitatu. Uongozi wake wenye haiba
ya kuvutia uliwatia moyo wanaume na wanawake, vijana na wazee, nchini
Marekani na ulimwenguni kote.

 (Kulia) Balozi wa Marekani nchini Michael L. Retzer alimtunukia Mzee Kawawa tuzo ya kumuenzi Dk. Martin Luther King inayojulikana kama Martin Luther King Jr. Drum Major for Justice Award.
(Kulia)Balozi wa Marekani nchini Michael L. Retzer alimtunukia Mzee Kawawa
tuzo ya kumuenzi Dk. Martin Luther King inayojulikana kama Martin Luther
King Jr. Drum Major for Justice Award. (January 23, 2007).  
(Kushoto) Mke wa Mzee Kawawa, Mzee Kawawa, Rais mstaafu Ali Hassan
Mwinyi, Balozi Retzer na Mwenyekiti Mfuko wa Mwalimu Nyerere, Salim
A. Salim.